Mch NAFTAL MSOLOKA AWA MWINJILISTI KITAIFA EAGT.

Waumini wa kanisa la EAGT Pangani mjini mnamo tarehe 26Nov2017 waliamua kufanya sherehe ndogo inayolenga kumshukuru MUNGU kwa kiongozi wao wa kanisa hilo Mch NAFTAL MSOLOKA kuwekewa mikono kuwa mwinjilisti wa taifa.

Aawali akitoa maelezo ya shughuli hiyo fupi Mzee wa kanisa na Katibu wa kanisa hilo Dr Josephat Makombe amesema kanisa hilo linamuunga mkono Mch Msoloka kwa kila atakokokwenda katika kazi ya kumtumikia MUNGU aliyemuita.

“lengo la sherehe hii fupi ni kumshukuru MUNGU kwa mchungaji wetu kuwekewa mikono na askofu mkuu kuwa mwinjilisti wa Taifa nasi tuko pamoja nawe katika kukuunga mkono kila uendako kufanya kazi ya MUNGU na tunakuahidi kama kanisa tuko nyuma yako” alisema Dr Makombe.

“kama kanisa sasa kwa hatua uliyofikia tunakushauri uanze harakati ya kutafuta pasport ya kusafiria kwani tunaamini kuwa sasa utakuwa na kibali cha kwenda hata nje ya mipaka ya Tanzania  na afrika mashariki kwa ujumla na kwenye hili tuko pamoja nawe, pia tunakushauri uanze mazoenzi ya kujifunza lugha za kigeni ili iwe rahisi katika kufanya mawasiliano huko uendako” aliongeza Dr Makombe.

Katika kumtakia kumtia moyo kiongozi huyo ambae ni Mwinjilisti Kitaifa kwa sasa Vijana, kinababa, kinamama na watoto wamesema katika kipindi ambacho hatukuwepo kanisani humo asifikirie u ya waliobaki kuwa watabakije ila ajue kuwa wako  pamoja nae katika maombi muda wote ili kufanikisha kazi ya Mungu.


Tazama baadi ya picha kwenye tukio hilo.

 Mch Naftal Msoloka akiingia kanisani.


waumini wa kanisa wakimlaki Mchungaji Msoloka.


Mch Naftal Msoloka akiwa na Mkewe 

Baadhi ya waumini wa kanisa


Dada Joyce akifungua zawadi ya mama mchungaji kwa niaba ya kanisa.


  Kijana John kisiwa akifungua zawadi ya Mchungaji kwaniaba ya kanisa.

.......................................
tembelea Youtube chanel yetu kuona mahubiri ya Mch Naftal Msoloka kwa kuandika EAGT PANGANI. 
usisahau ku-subscribe.
Latest
Previous
Next Post »