Maafisa wa serikali nchini Somalia, wamesema mwanachama wa cheo cha juu wa kundi la al-Shabaab Mukhtar Robow amejisalimisha kwa serikali.
Robow alijisalimisha pamoja na wapiganaji wake katika mji ulio kusini magharibi mwa Hudur.
Bw. Robow alikuwa Naibu Kiongozi wa al-Shabaab na msemaji wake kabla ya kutofautiana na kundi hilo miaka minne iliyopita.
Mwezi Juni, Marekani iliondoa zawadi ya dola milioni tano dhidi ya Robow ambaye bado anaaminika kuendelea na shughuli zake kama mwanamgambo
Sign up here with your email