Kwa nini wanawake wamekuwa wakitumia #MeToo kwenye Twitter

Alyssa Milano
Wanaume na wanawake kutoka maeneo mbalimbali duniani ambao wamenyanyaswa kijinsia wamekuwa wakisambaza habari zao katika mitandao ya kijamii wakitumia alama ya #Metoo kuonyesha viwango vya unyanyasaji wa kinjinsia ulivyokithiri.
Hatua hiyo inafuatia madai ya unyanyasaji dhidi ya mtayarishaji wa filamu katika Hollywood Harvey Weinstein.
Zaidi ya wanawake 20 akiwemo nyota wa filamu Angelina Jolie, Gwyneth Patltrow na Rose McGowan wametoa malalamishi dhidi yake ikiwemo ubakaji na nunyasaji wa kingono.
Wienstein amesisitiza kuwa uhusiano wa kingono aliokuwa nao ulikuwa umeruhusiwa na pande zote.
Tangu madai hayo kufichuliwa watu wengi maarufu wametumia mitandao ya kijamii kuliangazia swala la unyanyasaji wa kingono huku wengine wakielezea unyanyasaji waliopitia.
Wito huo unaotolewa chini ya #MeToo umetumiwa zaidi ya mara 200,000 tangu Jumapili usiku.
Neno hilo lilipata nguvu baada ya nyota wa filamu Alyssa Milano kuwataka waathiriwa wa unyanyasaji wa kingono kuwataka waathiriwa wa unyanyasaji wa kingono kujitokeza ili kuonyesha umoja.
Previous
Next Post »