Kwa nini Zimbabwe ina 'Waziri wa WhatsApp

Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe alipotangaza kwamba ameunda wizara mpya ya kuangazia usalama mtandaoni na kutambua hatari pamoja na kuchukua hatua, raia walianza utani. Kuna ilani bandia iliyoanza kuenezwa mtandaoni ambayo ilikuwa na sahihi bandia pamoja na nembo ya waziri huyo mpya Patrick Chinamasa. Katika barua hiyo, waziri huyo alikuwa amewaagiza wanachama wote wa makundi ya WhatsApp kuhakikisha wamejisajili katika wizara hiyo kufikia Novemba. Kwenye sahihi yake, palikuwa pameandikwa "Kwa Kutumia Mamlaka ya Mtandaoni Niliyopewa." Lakini utani huo sasa umepungua, na raia wa Zimbabwe sasa wanajadili matokeo ambayo wizara hiyo itakwua nayo kwa uhuru wa raia - sana uhuru wa kujieleza.
Previous
Next Post »