Marekani yataka utulivu baada ya wanajeshi wa Iraq kuingia Kirkuk

Marekani imeombakuwepo utulivu baada ya wanajeshi wa serikali ya Iraq kuteka mji wa Kaskazini mwa Iraq wa Kirkuk na vituo muhimu kutoka kwa wakurdi.



Iraqi forces flash a victory sign while driving past an oil production plant near Kirkuk. Photo: 16 October 2017

Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani Heather Nauert amezitaka penda zote kuzuia makabiliano zaidi.
Wanajeshi wa Iraq walielekea Kirkuk wiki tatu zilizopita, baada ya eneo la Kurdistan kuandaa kura ya maoni ya uhuru iliyokumbwa na utata

Lengo lao ni kuteka sehemu zilizo chini ya udhibiti wa wakurdi tangu Islamic State wadhibiti eneo hilo.
Wenyeji wa maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa wakurdi ukiwemo mji wa Kirkuk, kwa wingi waliunga mkono kujitenga kutoka Iraq wakati wa kura ya tarehe 25 mwezi Septemba.

Licha ya mji wa Kirkuk kuwa nje ya eneo la Kursistan, wapigaji kura wa Kurdistan walio mjini humo waliruhusiwa kushiriki kura.
Waziri mkuu wa Iraq Haider al-Abadi aliitupilia mbali kura hiyo na kuitaja kuwa iliyo kinyume na katiba.
Previous
Next Post »